|
CONGREGATION
MELECH YISRAEL OF TORONTO |
||||
|
||||
|
|
|
Bila shaka Yisraeli (Israeli) walihitaji kuheshimu wadhifa wa Kohen HaGadoli (Kuhani Mkuu), lakini hiyo haikumaanisha kwamba alikuwa na kiwango kikubwa cha kibinadamu kuliko Am Yisraeli (watu wa Israeli) wengine wote. Sisi vilevile tunahitaji kuheshimu nyadhifa za marabbi wetu, wachungaji na mapadri, lakini nyadhifa zao hakika haziwatengi wao na ubinadamu pamoja na udhaifu wake, kama vile washarika wengine wote wanavyoupitia. Hii inatuleta katika somo la Miriam (Maria) mama wa Yeshua. Uri (Luka) {1:48} Kwa kuwa Amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mwenye hali ya chini. Hivyo tangu sasa vizazi vyote wataniita mbarikiwa. Ni kweli kwamba HaShem alimpa Miriam nyadhifa iliyobarikiwa na yenye kuinuliwa kati ya wanawake. Walakini hiyo haikumfanya yeye awe zaidi ya wanadamu wengine wote na Andiko linashuhudia hilo. Uri (Luka) {2:21} Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina YESHUA, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla Hajachukuliwa mimba.{2:22} Siku zilipotimia za Miriam kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Moshe (Mose), wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerushalyim (Yerusalemu) ili Wamweke mbele ya BWANA; {2:23} (Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: "Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana;"){2:24} Na walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya BWANA. Kwa kiwango ambacho Miriam alibarikiwa hakikumfanya yeye atengwe kutozifanya mitzvot (amri) za Torati. Mwanamke anahesabiwa kuwa na unajisi wa kiibada siku thelathini na tatu baada ya kumzaa mtoto wa kiume.Huu ndiyo ukweli uliokuwepo kuhusu Miriam japo kuwa mwanae alikuwa ni Yeshua, Mwana wa M-ngu. Vayikra / Walawi {12:2} Waambie bnei Yisrael (wana wa Israeli) hivi: Mwanamke akipata mimba, akajifungua mtoto wa kiume, atakuwa najisi kwa muda wa siku saba kulingana na siku zake zihusikanazo na hali ya wanawake. {12:3} Mtoto huyo atatahiriwa govi lake katika siku yake ya nane. {12:4} Kisha mama mtoto ataendelea kuwa najisi kwa muda wa siku thelathini na tatu. Wakati huo, kamwe asiguse chochote kilichowekwa wakfu wala kuingia mahali patakatifu mpaka siku za kutakasika kwake zitakapotimia. {12:6} ¡°Siku za kutakaswa kwake zitakapotimia, iwe amepata mtoto wa kiume au wa kike, atamletea kuhani mlangoni mwa hema la makutano mwanakondoo wa mwaka mmoja kwa ajli ya sadaka ya kuteketezwa na kinda la njiwa au hua, kwa ajili ya dhabihu ya dhambi: Haiwezi kuwa dhahiri ya hivi, kwamba HaShem hana ustahivu na watu zaidi ya ukweli wa kwamba, mama wa Mwana wa M-ngu alikuwa na unajisi wa kiibada na ilimpasa kupitia taratibu zote za utakaso kama zilivyoorodheshwa katika Torati, kabla ya kuingia katika Bet HaMikdash (Hekalu). Hata Yeshua, katika ubinadamu Wake, alikuja kutumikia na siyo kutumikiwa. Andiko liko wazi kabisa kwamba Aliyaendesha maisha Yake yote kwa kuiangalia Torati. Nafikiri ni jambo jema kwetu sote, bila kujali wadhifa wetu wa kijamii, kidini au kiuchumi, kuweka moyoni yale ambayo tunaonyeshwa hapa katika Parasha Tzav. HaShem hana ustahivu na mtu na sisi sote tunahitaji kutumikiana kwa unyenyekevu. Hakuna hata mmoja wetu ambaye yuko juu ya kutotenda dhambi na sisi sote tunahitaji korban. Kohellet (Mhubiri) {7:20}"Hakika, hakuna mtu mwadilifu duniani atendaye mema daima bila kutenda dhambi." Orodha ya masomo ya wiki hii:
YYYYYYYYYYYY (Jina la BWANA Libarikiwe) Rabbi Jack (Ya'acov) Farber |
Site
Design Copyright © 1999- Karl D. Baca All rights
Reserved |