CONGREGATION MELECH YISRAEL OF TORONTO
Usharika wa Melech Yisrael, Toronto, Canada - Kehilat Melech Yisrael, A Messianic Jewish Torah Observant Congregation, in Toronto, Canada / קהילת מלך ישראל, קהילה משיחית יהודית שומרת בתורה, הנימצאה בטורונתו, קנדה

פרשות השבוע - Parashot HaShavua

 Masomo ya Biblia Kwenye Mtandao

ENGLISH / ESPAÑOL / PORTUGUÊS / ITALIANO / FRANÇAIS / MAGYAR / KISWAHILI / / 한국어 / РУССКИЙ / עברית

Masomo ya wiki hii

YHome
YMonthly News Letters
YServices & Special Activities
YLocation Map
YWho we Are
YMission Statement
YWhat is Messianic Judaism?
YCMY Academy Day School
YBooks of Life Catalogue
YRebbetzin Corner
YLinks
..

Y Our E mail
Y Our ICQ Is # 79381635

.

  Jiunge na kundi la email
  

Masihi Myahudi

* DO WE WANT MASHIACH NOW?
FALSE MESSIAHS - TRUE MESSIAH
DO YOU WANT MASHIACH NOW?

UNTIL MASHIACH RETURNS

מתשובה למשיח לגאולה במהרה בימינו. זכריה י"ב:י'
ברוך הבא מלך המשיח!

אני מאמין באמונה שלמה בביאת המשיח ואף על פי שיתמהמה עם כל זה אחכה לו בכל יום שיבוא.

Radio Melech HaMashiach - רדיו מלך המשיח; a Messianic Jewish Radio Station on the Internet.

ישועה וגאולה אמיתית לכל ישראל.

פרשת השבוע צו
Parashat Tzav / Amuru

Y Vayikra / Walawi 6:1-8:36
Y Yermiyahu / Yeremia 7:21-8:3, 9:22-23
Y Mal'achi / Malaki 3:4-24
Y Messianic Jews / Ebrania 8:1-6
Y Kutoa Nakala safi (Bonyeza)
Y שבת הגדול / Shabbat HaGadol
Y Kuchangia huduma (Bonyeza)

“Neno lako nimelificha moyoni mwangu ili nisikutende dhambi” פרשת השבוע צו / Prashati HaShavua Tzav / Amuru; Usharika wa Melech Yisrael, Toronto, Canada
Shiur / Masomo
5765
5766 Shiur / Masomo (
Bonyeza)
 

Neno lako nimelificha moyoni mwangu ili nisikutende dhambi

Parsha hii imenishangaza! Ni vipi Moshe (Musa) aliweza kuzikumbuka taratibu zote hizi? Aliwezaje kufanya kila kitu kikamilifu na kukamilisha kila kipengele cha mwisho, kufuatana na maelekezo ya HaShem (BWANA) na labda masaa na hata masiku kabla? Mtu huyu aliwezaje kukumbuka haya yote?

Sasa siwezi kunukuu Parsha yote ili kuelezea kumbukumbu yote ya utekelezaji uliyohusika, hatahivyo nimechagua kisehemu kimoja ili tukisome kuona maelekezo ya kina Moshe alibidi ayakumbuke na kuyatenda.

Vayikra (Walawi) {8:10} Moshe alichukua mafuta ya upako, na alipakaa hema na vyote vilivyokuwamo ndani, na alivitakasa. {8:11}Alinyunyizia juu ya mitzbeach (madhabahu) mara saba, na alipakaa mitzbeach na vyombo vyake vyote, na beseni na kitako chake, alivitakasa. {8:12} Alimiminia mafuta ya upako kichwani pa Aharon, na alimpakaa, ili kumtakasa. {8:13} Moshe aliwaleta wana wa Aharon, na aliwavisha vimau , na aliwafunga kwa mishipi kiunoni, na aliwazungushia vilemba kichwani; kama HaShem alivyomwamuru Moshe. {8:14} Alimleta ngo’mbe dume wa dhabihu ya dhambi: na Aharon na wanawe waliweka mikono yao juu ya kichwa cha ngo’mbe dume wa dhabihu ya dhambi. {8:15} Alimchinja; na Moshe alichukua damu, na kuiweka na vidole vyake juu ya pembe kuzungukia mitzbeach, na aliitakasa madhabahu, na alimiminia damu katika kitako cha madhabahu, na aliitakasa, na kufanya Kapparah (Kifuniko/Upatanisho) kwa ajili yake. {8:16} Alichukua mafuta yote yaliyokuwamo ndani, na yaliyofunika maini, na mafigo mawili, na mafuta yake; na Moshe aliyachoma juu ya madhabahu. {8:17} Lakini ngo’mbe dume, na ngozi yake, na nyama yake, na samadi yake, alizichoma na moto inje ya kambi; kama HaShem alivyomwamuru Moshe. {8:18} Alimtoa kondoo dume wa olah korban (uteketezaji wa kukaribia / dhabihu): na Aharon na wanawe waliweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo dume. {8:19} Alimchinja; na Moshe alinyunyizia damu kunzungukia juu ya mitzbeach. {8:20} Akamkata kondoo dume vipande-vipande; na Moshe alichoma kichwa , na vipande, na mafuta. {8:21} Aliosha sehemu za ndani na miguu kwa maji, na Moshe alimuchoma kondoo dume wote juu ya madhabahu: alikuwa ni olah korban kwa harufu tamu: ilikuwa ni korban iliyoteketezwa na moto kwa HaShem; kama HaShem alivyomuamuru Moshe. {8:22} Alimtoa kondoo dume mwingine, kondoo dume wa wakfu: na Aharon na wanawe waliweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo dume. {8:23} Alimchinja; na Moshe alichukua damu yake, na aliiweka juu ya incha ya sikio la kulia la Aharon, na juu ya kidole gumba cha mkono wa kulia, na juu ya gumba la mguu wa kulia.

{8:24} Aliwaleta wana wa Aharon; na Moshe aliweka sehemu ya damu katika incha ya masikio yao ya kulia, na juu ya madole gumba ya mikono yao ya kulia, na juu ya magumba yao ya miguu yao ya kulia: na Moshe alinyunyizia damu kuzungukia juu ya mitzbeach. {8:25} Akachukua mafuta, na mkia wa mafuta, na mafuta yote yaliyokuwapo ndani, na vifuniko vya maini, na mafigo mawili, na mafuta yake, na paja la kulia: {8:26} na kutoka katika kikapu cha mikate isiyo chametz (isiyochachuliwa), iliyokuwepo mbele za HaShem, alichukua keki moja isiyo chametz,na keki moja ya mkate uliotiwa mafuta, na chapati maji,na aliviweka juu ya mafuta, na juu ya paja la kulia: {8:27} na aliviweka vyote juu ya mikono ya Aharon, na mikono ya wanawe, nao wakavipunga mbele ya HaShem dhabihu ya kupunga. {8:28} Moshe alivichukua vyote kutoka katika mikono yao, na alivichoma vyote juu ya mitzbeach juu ya dhabihu ya olah: vilikuwa ni harufu tamu ya kuweka wakfu: ilikuwa ni korban ya kuteketezwa na moto kwa HaShem. {8:29} Moshe alichukua kifua, na alipungia mbele za HaShem dhabihu ya kupunga: ilikuwa ni sehemu ya Moshe’ ya kondoo dume wa wakfu; kama HaShem alivyomuamuru Moshe.

Inashangaza, au siyo? Naamini Moshe aliyafanya haya yote kutokana na kumbukumbu yake tu! Labda utasema Moshe aliyaandika yote HaShem alimwelekeza kufanya na kutenda kila jukumu kufuatana na kuangalia maelekezo aliyoandika. Yaani alifuata maelekezo aliyopewa na HaShem pamoja na vielelezo kamili mithili ya vile tunafuata maelekezo ya kampuni katika kuunda fanicha tuliyonunua kama vipande-vipande vya kuunganisha pamoja, sawa? Hapana! Vifungu tulivyokwisha visoma ni baada ya tukio, viko katika nyakati iliyopita. Tunasoma yale ambayo Moshe alikwisha yafanya. Ilikwisha tendeke wakati haya yameandikwa. Je, Moshe aliwezaje kukumbuka yale yote ya kutenda, hasa ukitafakari kipengele kikuu na madhara yaliyofuatia kwa makosa yeyote?

Nadhani jibu liko katika ukweli wa kwamba wakati HaShem alimuamuru Moshe, yeye hakulichukulia kiepesi jambo lolote aliloambiwa na HaShem. Kila neno lililotoka mdomoni mwa BWANA, Moshe alijitahidi kujifunza, kukumbuka na kulitimiza kikamilifu. Je, Moshe alikuwa na uweza Fulani usio wa kawaida kukamilisha hili? Kiudhahiri siyo, maana alikuwa ni mtu wa kawaida tu!

Wengi wetu tuna matatizo ya kukumbuka amri za HaShem kutoka wakati mmoja hadi mwingine. Je, inamaanisha zinaburuga fikra zetu kutoweza kushika maagizo na masharti haya? Wangapi kati yenu mnayesoma drash (tafsiri) hii mmeajiriwa na kampuni yenye karatasi la muongozo lenye sera na taratibu za kampuni? Je, haikubidi kujifunza hizi sera na taratibu kwa ajili ya utendaji bora wa kazi yako? Je, kuna madhara yeyote iwapo hutafuata kikamilifu hizi sera na taratibu? Je, unanipata ninaelekea wapi? Tutachukua muda kujifunza na kukumbuka sera na taratibu zinazohitajika tulipoajiriwa, lakini ikija kwenye Torati ya HaShem, tunapuuzia mtazamo wote wa kukumbuka amri Zake na hivyo tunapendelea kukubali dhana isiyo sahihi inayosema amri zote zimefutwa na Yeshua. Hakuna haja ya kujifunza au kukumbuka yeyote ile, sawa? Cha kuchekesha ni kwamba hivi sivyo Daudi Melekh Yisrael (Mfalme wa Israeli), mwana zaburi anatuelezea. Yeye alifanya sawa kabisa kama Moshe alifanya na hakika alijihusisha katika kukariri Torati ya HaShem katika maisha yake.

Tehillim (Zaburi) {119:1}Wamebarikiwa wasionajisika katika njia, watembeao katika Torati ya HaShem. {119:2} Wamebarikiwa wazishikao shuhuda Zake, na wamtafutao Yeye kwa moyo wao wote. {119:3} Pia hawafanyi maovu: wanatembea katika njia Zake. {119:4} Umetuamuru tushike miongozo Yako kwa bidii. {119:5} Ee kama njia zangu zingeongozwa kushika masharti Yako! {119:6} Ndipo sitaaibika, ninapokuwa na heshema kwa amri Zako zote. {119:7} Nitakusifu Wewe na moyo uliyo na unyofu, nitakapokuwa nimeisha jifunza hukumu Zako ongofu.. {119:8}Nitashika masharti Yako: Ee usiniache mimi mbali. {119:9} Ni kwa vipi kijana ataitakasa njia yake? Kwa kuwa makini kulingana na Neno Lako. {119:10} Kwa moyo wangu wote nimekutafuta Wewe: Ee usiniache ni tangetange mbali na amri Zako. {119:11} Neno lako nimelificha moyoni mwangu, ili nisikutende dhambi. {119:12} Umebarikiwa Wewe, HaShem: nifundishe masharti Yako.

Je, umelificha Neno la HaShem moyoni mwako ili usimtende dhambi? Hakika Moshe alifanya, HaMelekh (Mfalme) Daudi alifanya vile-vile, haitupasi nasi tufanya sawa sawa badala ya kinyume chake?

YYYYYYYYYYYY
Baruch HaShem
(Jina la BWANA Libarikiwe)
Rabbi Jack (Ya'acov) Farber


Site Design Copyright © 1999- Karl D. Baca All rights Reserved
Congregation Melech Yisrael; 272 Ranee Ave. Toronto, Canada. M6A-1N6 Tel: 416-785-7612 - Fax: 416-785-9414
This site is maintained by the faithful support of its contributors. Donate online; Join our free e-mail group (Here)
A Torah Observant Messianic Jewish יהודים משיחים Congregation, Toronto, Ontario, Canada / Services in Spanish / En Español e Ingles.
An ever changing Messianic Jewish website till King Mashiach Yeshua comes back!!!
אנחנו רוצים משיח עכשיו  / МЫ ХОТИМ МАШИАХА СЕЙЧАС
WE WANT MASHIACH NOW / QUEREMOS AL MASHIAJ YA
יחי אדוננו מורנו ורבינו מלך המשיח לעולם ועד
Moshiach Now

ישוע המשיח