|
CONGREGATION
MELECH YISRAEL OF TORONTO |
||||
|
||||
|
|
|
Wanyama walizuiwa kujiendea sehemu yeyote karibu na mlima, na kutokutii kokote kwa aidha mwanadamu au mnyama kulimaanisha kifo hakika. Aharoni na wale walioambatana naye waliruhusiwa tu nusu ya njia kufikia juu milmani, wakati Moshe peke yake, mtu mmoja kati ya wanaume zaidi ya laki sita, aliruhusiwa kupanda hadi juu. Inachekesha kwamba hakuna hata neno moja katika Andiko linalomkataza yeyote asizurure Hari Sinai baada ya Shekinah ya HaShem kuondoka milmani, na tunaona bnei Yisraeli wakihama kambi kuelekea sehemu nyingine baada ya hapo. Unaweza kuwa na uhakika kwamba wanyama walianza kuwa malishoni kwenye miteremko yake na wachungaji wahamaji walikuwa wakizurura kwa uhuru tena juu yake pamoja na mifugo yao. Unaona, hakuna kitu chochote kitakatifu na mlima, ulikuwa ni mlima tu! Muda tu ambao Hari Sinai ulikuwa mtakatifu, ni wakati HaShem alikuwapo pale. Zaidi ya hapo ulikuwa ni mlima tu, na bado ni mlima tu popote utakapokuwa! Maana siyo mlima ambao ni mtakatifu bali ni HaShem. Siku hizi watu wengi wanafanya rabsha kubwa kuhusiana na 'Temple Mount' (Mlima wa Hekalu). Kuna tangazo kubwa katika lango la Mlima, mara ukitoka Kotel HaMaaravi (Ukuta wa Magaharibi), ambao unamwaonya yeyote aliye Myahudi asipande juu ya Mlima, asije kwa makosa akakanyaga katika ardhi ambayo ilishikilia Kadosh HaKodashim (Patakatifu pa Patakatifu). Sasa sitaki kuwa mtu asiye mstahivu na wala siyo nia yangu kukebehi; walakini, hakuna kitu chochote kitakatifu, hakuna uwakfu wowote kuhusiana na 'Temple Mount', kama Bet HaMikdash (Hekalu) halipo pale na zaidi kama uwepo wa HaShem hauko, yaani Shekinah Yake haiko ndani ya Bet HaMikdash. Mezuzah (kiboksi kidogo juu ya nguzo ya mlango wa nyumba), siyo takatifu tu kwa sababu kina kigombo chenye kisehemu cha Torati iliyoandikwa kwa mkono; Biblia siyo takatifu kwa sababu tu ina Neno la M-ngu; hakuna kitu kinachoitwa mafuta matakatifu ya upako au maji matakatifu, kama hakuna Bet HaMikdash pamoja na uwepo wa Shekinah wa kunyunyizia juu yake.Hebu tukubaliane na ukweli; hakuna kitakatifu isipokuwa HaShem. Sehemu zinakuwa takatifu tu kama Uwepo wa Kimungu uko pale na vitu vinakuwa vitakatifu kama vinatumika kuhudumu uwepo Wake. Au sivyo ni vitu tu na ni sehemu tu, yaani wino na karatasi tu. Wakati Melekhi (Mfalme) Yeshua HaMashiakhi anarudi, Atalijenga Bet HaMikdash na kufanya maskani yake pale, na utakatifu wa hapo awali wa Bet HaMikdash utarejeshwa kwa Yisraeli na ulimwenguni. Yeshayahu (Isaya) 66:23 - "Katika kila sikuku ya mwezi mpya (kuanzia mwezi mmoja wa Kiibrania hadi mwingine), na katika kila siku ya Shabbati (Sabato), binadamu wote watakuja kuniabudu", asema HaShem.
YYYYYYYYYYYY |
Site
Design Copyright © 1999- Congregation Melech Yisrael All rights
Reserved |